Τετάρτη 29 Οκτωβρίου 2025

IBADA YA MTAKATIFU BABA YETU KOSMAS

 

 «Πνευματική φαρέτρα τοῦ Ὀρθοδόξου Χριστιανοῦ»

YA MUTAWA DAMASKINOS GRIGORIATIS

MWALIMU YA KANISA ORTHODOKSE


IBADA YA MTAKATIFU BABA YETU KOSMAS

 MTUME MKUBWA WA KRISTU MU INCHI KONGO YA AFRIKA


TAFSIRI: MUTAWA DAMASKINOS GRIGORIATIS


UTUME YA KANISA ORTHODOKSA

JIBO YA KIASKOFU KATANGA

KOLWEZI KONGO

 2018

 

IBADA KIDOGO YA MANGARIBI

Tunasimama pa ma shahiri wa ine na tunaimba wimbo wa ine

Sauti ya ine.Mfano : Os genneon en martisin

 

Mwalimu mwenye pumuzi wa Mungu,  tegemeo ya Kanisa,  alimasi yenye kuangazwa katika ma fazila ya uzima utawa, tumusifu Kosmas musisahauliwa, chipuko ya inchi Ungiriki na johari ya Kongo, mushindaji mkubwa ya kanisa wa Kristu, aliyesabitisha imani mu Afrika kwa upendo takatifu.

 

Tangu umri ujana yako, ee Mutawa, ulikomaa katika maarifa na mafundisho yenye kikristu ya wababu wako, basi ulitayarishwa muda ya miaka mengi kwa kumuhubiri Muumba, aliyesemesha kwa Mitume wake waende pa inchi yote kwa kuhubiri Ufufuo Yake takatifu.

 

Ulijazwa, ewe mutukuzwa, kwa ma zawadi ya Roho Mtakatifu, tena ulichukuwa duniani mafundisho yenye mbalimbali kwa kazi ya Mungu. Hapo majeshi ya wanadamu ya Kongo walishangaa mfano yako, wenye uliwapenda kabisa na ulionyeshwa mu inchi yao kubwa mufuasi ya Mitume na mtumishi wa Mungu mwenye heri.

 

Nani kati ya wanadamu, ewe Mwalimu, ana zawadi takatifu kwa kusifu michoko mengi yako ya kila siku na usiku, mito ya majashu yako, na uzulumu ya kivukutu, yenye yote uliyevumilia,  ewe mwenye heri mpaka mwisho yako, Mtume Kosmas, kwa kupandisha mbego ya imani.

Utukufu kwa Baba…Sauti ya kwanza.

Tangu umri ujana yako, ewe mwenye heri, ulichaguliwa toka Mungu, kwa kukataa kila zoezo ya kidunia na  shangwe kimbaya,  juu ya kutumwa kati ya wana kondoo ya Afrika kwa ushuhuda ya imani takatifu. Basi, ulifanyikwa mfuasi ya Mitume, ma siku hizi yenye mwisho ya dunia na ulijitoa katika roho yako yote kwa Kristo  Muchungaji wa kwanza. Tena, kwa ajili ya sadaka yako utume ulishuhudiwa muchungaji ya ma kondoo wenye akili na mujengaji ya ma Altari Matakatifu na ulibatiza ma elfu ya wanadamu ya Afrika, wenye uliwatoa kwa Kristu mpaka mwisho yako kwa kumwanga na damu yako kusifiwa. Basi, sisi wote wa ndugu, warafiki na wasaidizi yako tunasifu ukumbusho yako heshimiwa na tunakusihi usisimame kumuombea Mungu Mwema kwa wokovu ya ma nafsi zetu.

Sasa na siku zote…Theotokion.

Kwa sababu unapokea maombi ya wenye zambi na usizarau ombolezo ya wenye taabu, umuombee Huyu aliyezaliwa toka tumbo yako, ewe Mtakatifu kamili Bikira, kwa kutuokoa.

 

APOSTIKHA.

Sauti ya pili. Mfano: Ikos tou Efratha.

Simamisha malalamiko ya watoto wa roho yako, kwa ajili ya magonjwa yao, katika ombi lako, ewe Kosma, mwenye akili wa Mungu mtakatifu.

Shahiri: Mafundisho yao yalisikilika duniani kote na neno lake mpaka mwisho wa dunia.

Tembelea shamba takatifu wa Kristu ya Afrika nzima, ewe mwenye heri mara tatu, huku pahali inalala na mwili yako, ewe Mushindaji.

 

Shahiri: Ewe Bwana, wapadri wako wanavaa uhakikisho na watawa wako wanashangilia.

Pokea maombi letu, ewe Kosma, Mtume wa Kristu, baba ya waaminifu wa Kongo na mupatanishi yetu na musaidizi mkubwa.

Utukufu kwa Baba…

Salamu, ulieyonekana kati ya miaka yenye mwisho mu inchi ya Kongo ya Afrika, pahali ulihubiri Fumbo ya Utatu Mtakatifu.

Sasa na siku zote…Theotokion.

Ee Bikira wewe, wa pekee ni kitumaini na ulinzi, kimbilio na kifuniko na shangilio takatifu ya waaminifu wote.

 

Sasa Bwana….Mungu Mtakatifu…Nyimbo kutoka Ibada ya Magaribi kubwa. Na kuaga.

 

MU IBADA YA MANGARIBI KUBWA.

 

Kisha Zaburi ya namba 104, tunaimba Zaburi ya kwanza, inayoanzwa : Mwenye heri mtu… ». Kisha tunaimba wimbo ya Bwana nimekuita na kisha tunasimama pa ma shahidi wa site na tunaimba wimbo :

 

Sauti ya kwanza. Mfano : Ton ouranion tagmaton.

Kujeni warafiki ya karamu tumuimbie wote, Kosmas, Mtume mkubwa na mutungaji ya Kongo nzima. Huyu kama mutumishi mtakatifu wa Mwokozi alichoka kabisa sawa mutumishi wa Kristu, juu ya kufundisha watu wote ma fumbo ya imani Takatifu.

 

Leo wanafurahi wote makundi ya waaminifu na wanaimba katika furaha mashindano makubwa, michoko na mateso, ma gazabu, yenye yote aliyavumilia huyu mwalimu musifiwa wa Kanisa Kosmas, aliyetukuzwa kama tegemeo takatifu ya Afrika.

 

Salamu na wewe, mutumishi wa Rabi, mwenye ajabu, uliyetoa uzima yako, kama uvumba takatifu, kwa Muangalifu kamili na Muumba Mungu, kwa kuhubiri kabisa na kuokoa ma nafsi ya wenye Afrika, mwenye heri kutoka Mungu.

Sauti ya mnane. O tu paradoksu thavmatos.

O muujiza ya ajabu, sababu pa miaka yenye mwisho, ulionyeshwa, ewe padri mwenye hekima ya Mungu, muhubiri mwenye kabaila wa Neno Mungu na uliangaa katika mafundisho yako kundi ya watu wenye inchi Kongo na uliwaokoa. O ya kitoleo yasipo kusemwa yako ewe mtakatifu mwenye ajabu Kosma ; basi umuombe juu ya wale uliwaongoza Kanisani wa Kristu.

 

Ninyi wa ndugu wote, tuna kweli sisi muombezi mkubwa mbele ya Kristu, huyu mtakatifu Kosmas anayesikia maombi zetu bila uzarau. Kweli huyu alionyeshwa kama jiwe isiyojitengwa ya uzima utawa na mushindaji mkubwa, pahali na mwili yake inakaa kati ya waaminifu wenye Kongo na inawapa ma neema na tunzo ya wale wanakimbilia katika heshima na imani kwake.

 

Nani atahimidi bahari ya mateso yako, ewe mwenye hekima Kosmas, michoko ya ma usiku, ma taabu na matatizo juu ya kazi ya Kristu, yenye yote uliyavumilia mu inchi ya Kongo, pahali kama mlimaji ulipandisha mbego ya Orthodoksia shambani isiyo tena kuleta matunda ya kiroho, halafu sasa ma roho ya waaminfu wanaonyesha matunda ya uzima yao kitawa.

Utukufu kwa Baba…Sauti ya sita.

Siku Kuu yenye kusifiwa liliangazwa leo kati ya mipaka yote ya Orthodoksia. Ni ukumbusho heshimiwa ya muchungaji na Mwalimu ya kati ya Afrika, shahidi na padre Kosmas. Basi, kujeni warafiki ya ma siku Kuu na washindaji wenye yasipo muchoko ya Kanisa kwa kumusifu mtume mupya wa Kristu, aliyezarau na mwili yake na alijitoa kama sadaka iliyopokelewa ndani ya Shamba wa Kristu ya inchi Kongo. Basi, sababu tunatimiza ukumbusho yake tupaze sauti na kusema katika kitukufu: Salamu Kosma, mufuasi ya Mitume na mwalimu ya taifa mweshimiwa ya inchi Kongo. Salamu, rafiki wetu mupendwa kamili na muhubiri musiye na kuchoka ya imani takatifu. Salamu uliyetembea siku nba usiku, bila kupenda maugu yako na ulionekana usingi na nguzo ya imani kwa kusabitisha imani ya Orthodoksia mu Afrika. Basi, kwani unasimama na uwezo mbele ya Bwana, umusihi juu ya watoto wenye roho yako, warafiki, wa ndugu na watumishi wako.

 

Sasa na siku zote…Theotokion. Sauti umoja.

          Nani hatakuita wewe Mwenye heri, Bikira Mtakatifu kamili? Nani hataimba kuzaliwa kwa Mwana wako bila mume? Kwani Mwana wa pekee aliyeangaa mbele ya wakati kwa Baba, yeye vilevile alitokea kwa wewe uliyesafi, akitwaa mwili usiyosemwa; yeye ni Mungu sawasawa na hali yake, na akajifanya mtu  kwa kadiri ya hali ya watu kwa ajili yetu; yeye hagawanyike kwa uso mbili, lakini anajulikana kwetu katika hali mbili bila muchanganyo. Umusihi, ee Bikira mutaratibu na heriu daima, kwa murehemu nafsi yetu.

 

Kuingia. Mwangaza Upole…Prokimenon ya Siku na Masomo

 

Somo katika kitabu cha  Mezali tutasoma (sura 9,1-11)

Hekima amejenga nyumba yake, amechonga nguzo zake saba. Amechinja nyama zake, amechanganya divai yake, ametandika meza yake. Ametuma wajakazi wake, waende kulia kutoka mainuko ya mji: Aliye mjinga apite hapa. Anamwambia mpumbavu: Njoni mle mkate wangu, mukanywe divai niliyochanganya. Acheni ujinga, na mtaishi, na kuendelea katika njia ya ufahamu. Anayekaripia mwewnye zarau anamgeuza kuwa adui wake; anayemkemea mtu mwovu anajivutia matusi. Usimkaripie mwenye zarau, asikuchukie; umkemee mwenye hekima, naye atakupenda. Umpe mwenye hekima, naye atazidi kupata hekima; umfundishe mwenye haki, naye atapata elimu zaidi. Asili ya hekima: kumcha Bwana, kumjua Mtakatifu, ndiyo akili. Maana, kwa ruhusa yangu, siku zinazidishwa, na miaka ya maisha inaongezeka. Kama una hekima, una hekima kwa faida yako; kama una zarau, wewe peke yako utabeba azabu yake.

 

Somo ya ya Hekima ya Solomono tutasoma (sura 3,1-10)

Roho ya watu wanyofu zimo mkononi mwa Mungu, wala masumbuko hayatawashika. Machoni pa watu wapumbavu walionekana kwamba wamekufa, na kufariki kwao kulizaniwa kuwa msiba, na kutengwa kwao mbali nasi kulizaniwa kuwa upotevu; bali wao wakaa na amani. Watu wanawaza kwamba wanyofu hao wamepata azabu, bali wao wamepewa uzima wa milele sababu ya matumishi yao. Baada ya kupatilizwa kidogo, watapokea mema makubwa, kwa maana Mungu amewajaribu akawaona kuwa watu wema. Kama vile zahabu inavyojaribiwa katika moto, hivyo Mungu amewajaribu, amewapokea kama sadaka ya kuteketezwa. Wakati watakapoangaliwa na Mungu, wao watangara, watametameta kama ndini za moto zenye kuchoma manyasi. Watawahukumu mataifa, watawatawala makabila, naye Bwana atakuwa mfalme wao milele. Wale wanaomtumainia Bwana watafahamu ukweli, nao walio waaminifu watakaa karibu naye katika mapendo. Bali wapotevu wataazibiwa kadiri ya moyo wao, kwa kuwa walimzarau mwandilifu na kumwacha Bwana wao.

 

Somo ya Hekima ya Solomono tutasoma (Sura 4, mustari 7-15)

Ikiwa mwenye haki amekufa kabla ya wakati wake atakaa raha mustarehe. Kwa maana heshima ya uzee haihesabiki kwa maisha marefu, wala haipimiki kadiri wa wingi wa miaka. Bali ujuzi huheshimiwa na watu kama mvi, na maisha safi kama uzee. Mwenye haki alimpendeza Mungu, akawa amependwa naye; kwa kuwa alikaa kati ya wakosaji aliondoshwa. Alichukuliwa ili uovu usipate kubadili nia yake wala hila isipevushe roho yake. Kwa kuwa mapendezi ya uovu hupitilia mbali mambo mema; kuzunguzungu cha matamaa mabaya hupotosha moyo mnyofu. Aliyekamilika upesi, huyu ndiye aliyetimiza miaka mingi. Kwa sababu Bwana alipendezwa na roho yake, basi kwa ajili ya hiyo alimuchukua hima kati ya ulimwengu mwovu. Watu huona jambo hilo, lakini hawaelewi, wala hawafikiri sana kwamba neema na huruma (ya Mungu) huwafikia wapenzi wake na ulinzi na tunzo ni kwa wachaji wake.

 

L I T I A

Sauti ya kwanza

Salamu na shangwe muji ya Shahidi mkubwa Dimitrios, Tesaloniki, unayezaa matunda matukufu, watungaji ya ulimwengu nzima na wahubiri wakubwa ya mataifa. Salamu na wewe Monasteri ya Mtakatifu Grigorios ya Mlima Takatifu Athoni, pahali ulimupokelea huyu mtume mkubwa Kosmas, muchungaji ya ma elfu mengi ya waaminifu  na ulimufundisha na ulimuongoza katika mafundisho ya angazo ya Wapadri. Huyu muda ya miaka mengi alitumika mu inchi kubwa ya Kongo na alisabitisha Kanisa wa Mungu katika matendo, maneno na ma alama yenye ajabu na anamuombea Mungu kwa wokovu ya ma nafsi zetu.

 

Sauti ya pili.

Kujeni makundi ya Waorthodoksi, tumusifu katika mahimidi na wimbo yenye kiroho, sawa inafai, muhubiri wa Kristu, Kosma sawa nyota yenye kuangaa nyingi ndani ya inchi ya Kongo. Huyu, alitambuka mito na ma bahari kwa kufundisha wenye Afrika. Alivumilia mashtaki na mafukuzo, magumu na michoko yasipo hesabiwa kwa usabitisho ya Orthodoksia mu inchi ya Kongo. Basi, kama mufuasi wa kweli ya Mitume, alijitoa sawa sadaka takatifu kwa Bwana na anasihi juu ya ma nafsi zetu.

 

Sauti ya tatu.

Kila mji na kijiji ya jibo ya Katanga ya Kongo, lilitaelezwa daima mashindani na matendo yako, ewe mtawa mtume wa Kristu Kosma. Sawa baragumu ulisafiri kati ya kijiji ya pori kwa kutafuta na kitumaini vitu vya jengo na kisha yalionekana ma kanisa yaliyojengwa kwa wewe kama buyoka kati ya ulongo ya Kongo. Watu wote walishanga kwa hekima na utimizo ya matendo yenye nguvu yako. Kwa hivi walikusifu na walikuwa wote wasaidizi katika upendo ya utume yako kubwa na yenye kuchokwa kabisa.

 

Sauti ya ine.

Salamu mji ya Thessaloniki ya Ungiriki, mugini ya mushindani ya Enjili ya Kristu, Kosma mwenye ajabu. Salamu, monastery ya Mtakatifu Grigorio ya Mlima Athosi, sababu ulimukumbatia huyu Mtume na ulimuongoza njiani ya uzima utawa. Salamu na wewe, muji ya Kolwezi Kongo, unayechunga kama hazina yenye ajabu, maiti takatifu na yenye kuchoka na unaonyesha ma alama yake na miujiza ya huyu mtumihsi mufazili ya Mungu, mwenyte heri Kosmas. Salamu na wewe taifa ya Kongo, kwani unachunga mulinzi na muhubiri na nguzo musiyetengwa ya Imani takatifu. Basi, uzikae na uzaifu kwa kusikia mafundisho yake juu ya kupata daima utukufu ya uzima ya milele.

 

Utukufu kwa Baba…Sauti ya ine.

Hekima ya Mungu tangu umri udongo yako alikuchagua, ewe mutawa Padri, na alikuotesha kama muti muzabibu kati ya shamba Kati ya Afrika. Bila kuogopa mateso ya muda ya kila nyakati, ukamio ya magonjwa, mapigo ya wanyanganyi, ma huzuni kwa ajili ya warafiki na ya wenye aliwapenda, ulisimama kama mushindaji muhodari ya Kanisa na ulitoa vitu vyote kwa upendo ya Muumba na wokovu ya taifa Yake. Tena na mwili yako uliitoa kama sadaka kwa Bwana na ulitukuzwa kwa ma alama na miujiza na ulifanyikwa sawa malaika mutulizaji ya taifa ya Afrika na mwombezi ya sisi wote, wenye tunasifu katika na furaha ukumbusho yako takatifu.

Sasa na siku zote…Theotokion.

Linda watumishi wako ku hatari yoyote, ee Mzazi-Mungu na Bikira mbarikiwa, ili tukutukuze kama kitumaini ya ma nafsi zetu.

 

APOSTIKHA

 

Sauti ya tano. Mfano: Kheris askitikon

Salamu chipuko ya Ungiriki, johari yenye kabaila ya muji Thessaloniki, musaidizi ya Kongo, mwalimu mtakatifu na mweshimiwa ya Afrika nzima na Mtume, mupiganaji ya ma shetani, na adui ya ufumu, mwogozi musiye na kosa ya wale walindanganywa, uliyekombanisha katika neema ya Roho Mtakatifu, mitengo yoyote ya watumishi ya shetani na uliongoza wenye  giza njiani ya Mfalme wa wote, ewe Kosma mwalimu, utulivu na shangilio ya Afrika nzima.

 

Shahiri: Ewe Bwana, wapadri wako wanavaa uhakikisho na watawa wako wanashangiliwa.

Uliacha furaha yote ya dunia, utukufu na sifa inayotoka bio na ulikuja mu monasteri ya mtakatifu Grigorio ya Mlima Athosi, pahali, ewe mwenye hekima, ulijifunza muzike ya wimbo na ma desturi ya ma ibada yote na ma fumbo ya Liturgia Kimungu kwa kupanda nafsi yako na neema takatifu. Basi, ulichukua vizuri mafundisho yote sawa angazo na ulionekana mu Afrika, mwalimu ya wakaaji pale ; sababu ulionyeshwa mwalimu mkamilifu ya wenye Afrika, na mchungaji wa roho, kweli ulitukuzwa kwa Mungu.

 

Shahiri :  Kifo ya Mtakatifu yake ni kusifiwa mbele ya Bwana

Sawa ulikuwa na mu nafsi zako upendo takatifu, kama nguvu isiyozimikwa, uliondoka ku inchi yako, ulishuka mu Afrika na ulifika mu inchi Kongo, ewe Padri. Pale, sababu ulichukuwa silaha ya neema wa Kristu, ulionekana nguzo ya waaminifu na mshindaji; tena ulibatiza kati ya maji ya mito, mataifa wingi, waliyokosa angazo ya Imani na uliwaongoza na upendo njiani ya mafundisho ya Kanisa, ewe Kosma, uliyeshuhudiwa mufuasi ya Mitume na johari kubwa.

 

Utukufu kwa Baba…..Sauti ya mnane.

Ewe Mutawa Padri,  ulimupenda kamili Kristu kwani ulijifunza vizuri mu monasteri ya Mtakatifu Grigorio ya Mlima Athosi. Kwa hivi katika baraka ya padri mkubwa yako Georgio, ulichukuwa cheo ya upandirisho na kuchunga sawa silaha ma shauri ya mtakatifu Baba wetu Paisios, ulitoka ku Mlima Takatifu, ewe Mweshimiwa. Basi, sawa kufuata shauria ya muchungaji wa roho yako askofu Timotheo, ulifika Kati ya Afrika kwa kutafuta kondoo mpotevu wa Mungu. Ulizarau kabisa uzima yako, ulijitoa kutenda upenzi takatifu na ulijenga ma kanisa kupita ya kumi. Tena ulifundisha na ulibatiza ma elfu mengi ya wale wenye Afrika. Basi, na Kristu, alikustahilisha, ewe mwenye heri kamili, kuchukua kitukufu ya ma zawadi mengi, kama mtumishi Yake mwema, juu ya kumuombea kwa wokovu yetu.

Sasa na siku zote….Theotokion.

Bikira usiyoolewa, mwenye kuchukua Mungu katika mwili, usiyosemwa, Mama wa Mungu aliye juu na bila doa, pokea usihi wa watumishi wako; wewe uliyeleta kwa wote safisho za makosa, sasa pokea ombi letu, na patanisha kwa ajili ya wokovu wa sisi wote.

 

Sasa Bwana, umuache…Mungu Mtakatifu…Na Wimbo (Apolitikia).

 

Sauti ya tano. Ton Sinanarkhon Logon.

Muhubiri mtakatifu Kosmas ya fasi Kati ya Afrika na mtume wa Kristu tumusifu sisi wote, aliyevumilia kabisa mateso ya Kristu na aliongoza Kwake makundi ya waaminifu mu inchi kubwa Kongo na anamusihi bila kusimama kwa wokovu ya ma nafsi zetu.

 

INGINE:  Sauti ya tatu. Tin oreotita.

Muhubiri mtakaitfu na Mtume Kosmas, aliyeongoza taifa isiyo na hekima njiani ya wokovu katika Enjili Takatifu na alimukikisha Bwana kabisa pa miaka hizizi yenye mwisho mu Afrika ya Katikati. Huyu, basi tunamusifu sasa, salamu shahidi na padri wa Kristu.

Theotokion.

Bikira Mzazi-Mungu tunakuimbia, wewe mupatanishi wa wokovu juu ya ukoo wetu;  katika mwili alipata Kwako, Mwana wako na Mungu wetu, alitaka kuteswa Msalabani, juu ya kutukomboa ku lufu, sawa Mpenda-wanadamu.

 

 

SALA YA ASUBUYI

 

KATHISMA YA KWANZA

Sauti ya kwanza. Ton tafon sou Sotir.

Ewe mwenye akili wa Mungu, ulitoka ku inchi ya kuzaliwa yako na ulishuka kati ya Afrika, pahali ulijikazwa kama muhubiri ya Imani na mujengaji mwenye kabaila ya makanisa; Hivi ulikokota wenye Afrika Paradizoni, ewe Kosma, urembo ya watawa na musaidizi mkubwa.

Utukufu kwa Baba…Sasa na siku zote…Theotokion.

Kwani, ewe Malkia, una uwezo mbele ya Muumba, sawa na Mama yake, unikomboe kwa maombi lako na simamisha zoruba ya ma tamaa ya nafsi zangu; tena unipe neema tele, juu anipatie Rabi Mwana wako raha rohoni mwangu pa hii uzima ya dunia.

KATHISMA YA MBILI

Sauti ya ine. O Ipsothis en to Stavro.

Kwa kutimiza amri ya Bwana, ulikuja mu Afrika ya inchi Kongo, pahali, ewe mwenye hekima, katika maneno yako na matendoiya imani ulionyesha utukufu ya Kristu Mfalme wetu na ulijenga ma Altari Mtakatifu mingi; basi ulionekena nguzo ya Orthodoksia na chombo ya imani kubwa.

Utukufu kwa Baba…Sasa na siku zote…Theotokion.

Ulitumwa, ewe Mama wa Mungu, toka Mungu, duniani, ile nyakati yalizambahwa matawala ya wazulumu ya dunia na ulifanyikwa, ewe Mwenye safi kamili, mlango ya wokovu, sawa ulimuzaa Mwana na Mungu wako. Huyu, basi, ewe Bikira, umusihi daima atusaidie na atuokoe ku mateso yetu.

 

KISHA POLIELEO. KATHISMA

Sauti ya mnane. Mfano; Tin Sofian ke Logon.

Ulikataa na upendo kimungu, ewe padri mwenye hekima, masubuko yenye dunia daima, na sawa ndege ya Muumba, ulikimbia kuingia  bandarini ya Mlima Takatifu, mu monasteri ya Mtakatifu Grigorio mwenye heri, pahali katika mashindano ya kiroho na sala ya kukesha na matendo mingi ulimutumikisha Bwana wako, ewe mtakatifu. Kisha ulisafiri mu Afrika kwa kumuhubiri Kristu na kupeleka pale, ewe Kosmas Mwalimu na muchungaji mwenye kuangazwa kwa Mungu, mafundisho ya wokovu na uzima ya milele.

 

Utukufu kwa Baba…Sasa na siku zote…Theotokion. Sauti umoja.

Nimeanguka kati ya mitengo yenye jaribu na ninateswa kwa woga ya wa adui wenye kuonekana na wasiyoonekana, tena kwa ajili ya makosa yangu yasiyohesabiwa; Basi ninakimbilia mu kivuko ya saidio na kifuniko yako, ewe Mwenye safi  kamili. Basi, sababu ewe Mtakatifu kamili, ulimuzaa Mwana wako, bila mbego, umusihi juu ya sisi watumwa mwako, amba wanakuhimidi bila kusimama, kwa ombi lako Mungu atupatie usamehe ya ma zambi zetu na kwa wale wanasujudu Uzazi wako, ewe Mwimbiwa kwa milele.

 

ANAVATHMI. Sauti ya ine:

Tangu ujana wangu, tamaa zenye kunishambulia zilinizunguka, lakini wewe, ee Mwokozi wangu, unilinde na uniokoe.

Adui wote wa Sayuni wanyamazishwe na Bwana kama nyasi yenye kuungua inapokauka.

Utukufu kwa Baba....

Roho yote inaishi kwa neema ya Roho Mtakatifu na inaishi na usafi wote kwa kuangaa sababu ya kuangazia dunia yote.

Sasa na siku zote...

Mawimbi ya neema yenye kunywesha kiumbe yote sababu ya kuchanua uzima yanachirizika kwa Roho Mtakatifu.

Prokimenon. Sauti ya Ine:

Mafundisho yao yalisikilika duniani kote. (mara pili)

Shahiri: Mbingu zinahadisia utukufu wa Mungu, anga inatangaza kazi ya mikono yake.

Mafundisho yao yalisikilika duniani kote.(mara moja)

Kila mwenye pumuzi amsifu Bwana (mara tatu).

Evangelio ya Yoane 10, 9-16

Mimi ni mlango: mtu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoa; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. Mwizi anakuja kuiba tu na kuchinja na kupoteza; mimi nimekuja ili wawe na uzima, tena waujaliwe kwa wingi. Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema atoa uzima wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, asiye mchungaji, wala mwenyeji wa kondoo, akimwona mbwa-mwitu anakuja, anawaacha kondoo, anakimbia; naye mbwa-mwitu anawakamata na kuwatawanya. Mtu wa mshahara anakimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara, nao moyo wake haushuruliki na kondoo. Mimi ni mchungaji mwema: nawajua walio wangu, nao walio wangu wanijua: vile kama Baba anavyonijua, nami ninavyomjua Baba; tena natoia uzima wangu kwa ajili ya kondoo. Nina kondoo wengine pia, wasio wa zizi hili: nao wale sherti niwaongoze, nao watasikiliza sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na mchungaji mmoja.

 

Somo ya Zaburi 50 (51)

Utukufu kwa Baba….Kwa maombezi ya Mtume, ee Murahimu…

Sasa na siku zote….Kwa maombezi ya Mzazi Mungu, ee Murahimu……

Unirehemu ee Mungu sawasawa…

Sauti ya sita

Lilimwanga neema ku midomo yako, ewe mutawa padri pa mipaka yote ya Afrika na wenye Afrika walifamia na namna ya siri Fumbo kubwa ya Orthodoksia. Kwa hivi ulitembea katika miguu yako yenye furaha pa fasi yote ya Afrika ya Kati, pahali ulihubiri matendo yenye ajabu wa Mungu. Basi, ulikokota ma elfu mingi ya mataifa wenye Afika mu kundi ya waaminifu wa Kristu. Tena ulijenga na ma Altari matakatifu na ma shule ewe mwenye heri. Na sasa pale mbinguni kwani unashangilia pamoja na Mitume wengine, umusihi Bwana daima atupatie neema na ufalme wa milele.

 

Shemasi ao Padri : Ee Mungu, okoa taifa yako na bariki uriti wako…

 

KANUNI YA WATAKATIFU

Nyimbo ya kwanza. Sauti ya mnane. Armatilatin Farao.

Ulichukua neema ya Roho Mtakatifu, ewe mwenye hekima, na ulimaliza kazi yako kwa kumwangisha na damu yako huku duniani ; hivi ulipanda mbinguni, pempeni ya Watakatifu wote ; basi unipe bahari ya neema ili kukuhimidi, sawa inafai.

 

Tangu umri utoto yako, ewe Mutawa, uliangazwa kwa neema takatifu ; hivi ulichukia tamaa ya kidunia na kila furaha yenye kimwili na ulikimbilia mu monasteri ya Grigoriu ya Mlima Takatifu, pahali katika matendo yako ulimufurahisha Mungu.

 

Sawa mutawa ya monasteri yako uliishi uzima takatifu, ewe mwenye hekima, na ulichukua wito kutoka mbingu ; kwa hivi na baraka ya mtakatifu mupya Paisios ulifika mu Afrika kwa kufanya na upendo kubwa tendo wa Mungu na wokovu ya wa ndugu wako.

Theotokion.

Ewe Bibi-Malkia, toka tumbo yako ilionekana wokovu na makundi ya wanadamu wingi walikokotwa kwa Mwana wako, aliyekuja duniani sawa Mungu na Mtu na aliponyesha magonjwa ya watu na alifurahisha kwa ujio yake ma roho ya watu wote.

 

Nyimbo ya tatu. O stereosas kat arkhas.

Furahini makundi ya waaminifu pa fasi ya ulimwengu nzima, na mumutukuze Kristo katika akili kimungu, kwani mu inchi ya Afrika, alijikazwa kama Goliathi, padri Kosmas, mfuasi ya Mitume na johari ya wapadri wote.

 

Nani ataweza kusema, ewe mletaji Mungu, michoko yako yenye uliyotenda ma siku na mu usiku zote? Kwani ulikataa kupumzisha mwili yako mpaka mwisho ya kumwanga damu yako, juu ya kusabitishwa muti ya Orthodoksia na kuzaa Matunda ya kiroho.

 

Ma muji ya Kongo nzima, sawa Kolwezi, Likasi, Bukama, Lwalamba na Lwena wanalalamika katika furaha, kwani waaminifu pale walichukua Imani takatifu na wanakushukuru kama Baba mtakatifu na mulinzi wao ya roho.

Theotokion.

Kwa ajili ya upendo ya wanadamu, alishuka, ewe Bikira, Mwano wako tumboni mwako na alichukua mwili sawa Mtu na Mungu; hivi alionekana duniani kwa kuleta kwa wanadamu njia ya wokovu na rehema kubwa.

 

KATHISMA. Sauti ya ine. Takhi prokatalave

Uliishi duniani, lakini ulikataa mitengo ya shetani, ewe mwenye heri ; basi hivi ulifanyikwa kweli chombo ya neema takatifu na uliwalikuwa kutenda kazi ya Nenno Mungu ; hivi ulikuwa muhubiri ya watu wa Afrika, mujengaji mkubwa na muchungaji yao na mwalimu mwenye hekima.

Utukufu kwa Baba…Sasa na siku zote…Theotokion

Makosa yangu tangu ujana ni mengi, lakini  nilikimbilia kwako, ewe Mwimbiwa kamili na kupiga magoti naomba usamehe ya matendo mabaya yangu, tena unipe neema nyingi ya Mungu, kwani paka hivi nifuate, ewe Malkia, njia ya kurudia na kuingia mu Ufalme wa mbingu.

 

Nyimbo ya ine. Si mou ischis Kirie.

Ewe mwenye heri, ulionekana kweli, makao takatifu na namna yenye ya mbalimbali, kwa hivi ulikabula utajiri ya ma fazila yako kati ya makundi ya waaminifu wako, pale mu inchi ya Kongo ya Afrika, pahali na mwili yako imezikwa.

 

Ma kunbdi mengi sasa ya Waaminifu wenye Afrika wanakimbilia kaburini pako na wanaomba neema takatifu, pamoja na uponyo ya ma taabu na usimamisho ya mateso yao. Kwa hivi, ewe Mletaji wa Mungu, uwapatie kwa watu wako saidio na angazo takatifu.

 

Ulitukuzwa pamoja na Wamalaika pale mbinguni, tena na makundi ya Watakatifu wote na Mitume wa Kristu, kwani na wewe, ee Mletaji Mungu, ulitoa katika roho yako kwa Kristu vitu vyote na ulionekana mwenye ustahili na Watakatifu.

Theotokion.

Salamu Mweshimiwa na Mzazi wa Mungu Mwimbiwa kamili, uliyezaa Mwokozi na Bwana na kimbilio ya Waorthodoksi ; kwa hivi wanafurahi juu ya kitumaini ya ufufuo ya kiroho na wanakushukuru, kama Mama wa Mungu na ukuta yetu isiyobomowa.

 

Nyimbo ya tano. Ina ti me aposo.

Ewe Padri kutoka kaburi yako, sawa chemchem ya uponyo yanatoka ma ishara na matunzo, moshi ya shetezo, ujio ya Wamalaika na miujiza; basi waaminifu wote wenye Afrika wanakushukuru na wanakufamia sawa mwalimu yao na mwombezi.

 

Sawa mtu mwenye akili, ulizarau makelele yenye dunia na vitu vya ovyo na ulijitoa kwa Muumba katika roho yako yako. Hivi ulifanyikwa nguzo ya wenye Afrika, mujengaji ya ma Altari Matakatifu mpaka kumwanga na damu yako kwa imani takatifu.

 

Sawa askari ulionyeshwa kweli mpaka mwisho ya uzima yako, na hivi ulitoa ma elfu mengi ya ma kondoo kwa Bwana ya jibo ingine, kwani ulijitoa kama sadaka kwa kuwapatia na mahubiri yako wokovu ya ma nafsi zao.

Theotokion.

Sababu, ewe Mama Mtakatifu, unakaa na uwezo mbele ya Huyu aliyekutukuza, usisimame kumuombea juu ya ubinadamu takatifu, kwani kweli wewe ni, ewe Bikira, kimbilio yetu na utuopoe toka kila kitu kimbaya.

 

Nyimbo ya sita. Ilasthiti mi Sotir.

Ma kundi ya wenye Afrika na majeshi ya wenye watu wa Kongo, kujeni sasa kumusifu Kosmas mtume, baba wa roho na mwalimu na mutumishi wa Rabi, wetu, aliyeweka usingi ya Orthodoksia mu Afrika.

 

Uzima yako, ewe baba mtakatifu, ilionekana sawa baragumu na iliangazwa kwa majengo ya matendo mengi, sawa ma Altari, ma shule yta watoto, obitalo yta wagonjwa na ma nduka ya watumishi wako.

 

Kweli inatukuzwa inchi ya Afrika na kabisa jibo ya Kongo kusini, sawa inakaa na hazina mwili yako takatifu, inayopona wagonjwa na inawapa kwa wote shangilio na matunzo mengi.

Theotokion.

Ninyi wa ndugu wote sawa inafai tupige magoti mbele ya Mwimbiwa kamili Malkia, na katika maombi yetu tumusihi atusaidie na tupate na sisi rehema kubwa kabisa ile siku ya uhukumu ya dunia.

 

KONTAKION

Sauti ya mbili. Ta ano ziton.

Kwa sababu ulimupenda Kristo tangu umri utoto yako, ewe Mwenye heri kamili,  ulimufuata katika upendo na ulisikia sauti yake kwa kutembea pa lupango ingine Yake juu ya kumuhubiri  kwa wokovu ya wale wanaishi ndani ya giza.

NYUMBA (IKOS).

Kwani, ewe padri Kosma, ulichukua ku umri utume yako  toka wazazi wako, waaminifu wa kweli, mafundisho yenye mbalimbali na utako kwa kumupenda Bwana. Basi, hivi ulikimbilia ku monasteri ya mtakatifu Grigorio ya Mlima Takatifu Athosi. Pale ulikomaa mu uzima kitawa na ulipokelea cheo ya upandirisho na baraka ya padri wa roho yako. Hivi, sawa kuchukua silaha ya kiroho na askari ya Kristu, ulikuja kati ya Afrika, bila kuangalia nyuma yako. Basi, katika michoko mengi ulijenga ma Altari ya Bwana, shule ya wanafunji, ma obitalo ya wagonjwa na ulijitoa sadaka kwa utukufu ya Mungu. Ulifuata mfano ya Mitume wa Kristu na uliacha na mwili yako pale mjini Kolwezi, pahali ni kaburi yako sawa moja kitoleo kubwa ya taifa ya Afrika nzima. Basi, na sisi wote kutoka Ulaya na Afrika tunakusifu katika heshima, kwani ulijitoa kwa wokovu ya taifa aliyeishi ndani ya giza.

 

SINAKSARI

Hii tarehe 27 ya mwezi januari, ni siku ya kifo kwa ajili ya musimbi njiani ya Mtume wa Yesu Kristu na shahidi Kosmas Grigoriatis, aliyekufa mu mwaka 1989. Hivi na leo tunashangilia sisi ukumbusho ya mwisho yake huku ya inchi Kongo.

 

Shahiri: Padri Kosmas, mutumishi wa Orthodoksia

na Mtume ya Afrika musiye na muchoko

Mu tarehe 27 ya mwezi Januari inasifiwa ukumbusho yake, katika wimbo sawa inafai na inalazimiswa.

 

Nyimbo ya saba. Theou sigatavasin.

Ulitoka, ewe musisahauliwa, ku kelele yote ya dunia na ulipitisha muda kidogo mu monasteri yako ya Mlima Athosi, pahali uliitwa kutoka mbingu kwa kutumikisha shambani ya Bwana mu Afrika, pahali ulipandisha mbego ya imani takatifu.

 

Unakaa, ewe Mutawa, mbinguni pahali unashangilia kabisa pamoja na Watakatifu Wamalaika na majeshi ya Mitume, pahali ulihesabiwa nao. Basi muimbie wimbo kwa Kristo kusema: Mungu ya Wapadri wetu ni mubarikiwa.

 

Taifa ya wakristu wanafurahi na wanakusifu katika wimbo ya heshima na shukrani; tena wote waaminifu ya Kongo wanakimbilia kaburini yako kusema nyimbo ya kukushukuru na kulalamika; Mungu ya Wapadri ni mubarikiwa.

 

Theotokion.

Ewe Bikira Mwenye safi kamili, kwani ulimuzaa Mungu, bila kusemwa, umusihi Mwana wako, kwani una uwezo mbele yake, juu katika maombi lako tupite na sisi kati ya ma hatari yote ya uharibifu kabisa na ile siku ya uhukumu yetu.

 

Nyimbo ya mnane. Eptaplasios kaminon.

Katika roho na mwili yako yote ulijitoa Shambani ya Bwana, pale ya Afrika, ewe Musisahauliwa kwa upendo yako iliyokuwa nayo tangu utoto yako. Basi ulichukua silaha ya kiroho na ulishuka mu jibo ya Kongo ya Afrika, pahali ulionyeshwa mutenda kazi mkubwa ya upendo, ewe mwenye akili wa Mungu.

 

Inafurahi kundi ya wanadamu, mataifa ya Afrika, watu ya muji ya kijiji ya jibo Kongo, kwani wana daima karibu yao kaburi na mwili yako sawa moja baraka kubwa, pahali wanapiha magoti mbele yako kukujulisha mateso na magonjwa yao. Basi mwanakushukuru na hivi wanakutoa wimbo ya shukrani kwako.

 

Salamu johari ya jibo Katanga, musaidizi ya mji Kolwezi na mutulizaji ya Lumbumbashi. Salamu mwalimu ya muji Kanyama, Tsiamula na Musonoi na ya kila muji na kijiji ya Kongo kusini, sababu ulifanyika mujengaji ya ma kanisa mengi, pahali inakuja wokovu ya wale watu wanakimbilia na imani.

Theotokion.

Ewe Malkia, utukumbuke sisi wote katika upatanisho yako na simama kama mulinzi na msaidizi yetu mbele ya kila uzulumu na taabu inayokuja kwa chuki ya muuaji ya kundi ya wanadamu shetani. Kwani tuko wamaskini ya kiroho na tunatumainia tupate neema yako kubwa, kwa uwezo yako.

 

Nyimbo ya Tisa. Eksesti epi touto o ouranos.

Ilionekana karamu kubwa ma siku hizi yenye mwisho ya dunia, ee warafiki wa karamu huku mu Afrika na ya kila jibo, pahali ma kundi ya Waaminifu waorthodoksi walipandisha wimbo mbele ya Mfalme na Muumba, juu ya kumushukuru aliyewapatia kama zawadi padri Kosmas, aliyetukuzwa katika maneno na matendo ya Kongo nzima.

 

Tunasifu mashindano yenye kiroho, ewe Mushindaji wa Bwana, usubuko yako isiyo na uzaifu juu ya kazi takatifu, ma safari yako siku na usiku, ma hatari na jotto ya jua ya Afrika, na matatizo yako na tunashangaa. Basi tunaulizwa, ni nani kweli ataweza kueleza na kuhesabia kitukufu ya matendo yako yenye ajabu, ewe Mweshimiwa?

 

Nilitimiza kipaswa katika heshima mbele yako kwa kusifu matendo yenye ajabu yako, mimi rafiki na mupendwa wako, ambaye ulimupenda tangu zamani; kwani unakaa na uwezo mbele ya Mfalme utukumbuke na sisi, wazazi na wandugu, warafiki, watumishi na watawa ya Mlima Takatifu kwa kupata na sisi wokovu ya ma nafsi zetu.

Theotokion.

Kama Mama wa Mkombozi, uliunganisha watu wa zamani na wa sasa kwa ajili ya Uzazi yako kubwa; basi na hivi pokea maombi na maombolezo yetu na utufunike wote katika Kifuniko yako, ewe Mwema, tena fukuza ukamio na ma shetani na okoa taifa anayelalamika kwakjo na huzuni rohoni mwake.

 

EKSAPOSTILARIO

Sauti ya mbili. Tis mathites sinelthomen

Kosmas mtume na mwanafunzi wa Kristu, chipuko ya mji Thessaloniki, johari ya Mlima Athosi tumuhimidi wote, sawa muhubiri ya Afrika, mujengaji mwenye kabaila ya ma Altari mengi ya Bwana, muzulumu na mupiganaji ya ma shetani, tena mulinzi ya wenye yatima na baba musiye na muchoko ya wamaskini.

Theotokion.

Ewe Maria mwenye kutukuzwa kwa Mungu, johari ya wakristiani, heshima ya ulimwengu, Mama ya waorthodoksi, pokea maombi yetu na fukuza zorumba ya ma tamaa yetu ; tena tuma jangwani mawimbi ya mawazo mabaya na utupe uponyo ya kila ugonjwa na kwa kila tamaa mbaya, ewe Mama wetu Mweshimiwa.

 

MASIFU

Sauti ya ine. Os genneon en martisin.

Makundi yote ya Afrika Kati na ya inchi Kongo, kujeni tumuhimidi Mtume Kosmas muhubiri mtakatifu mutukuzwa, na mwalimu ya Kanisa, sawa usingi ya wakristu wote, mulinzi mkubwa ya wajane na wamaskini ; tena tumusifu sawa rafiki ya Mwokozi aliyesabitisha katika michoko kitukufu ya Orthodoksia mu Kongo.

 

Ulishuhudiwa, ewe mwenye heri kamili, kama mushindaji ya Imani, mushindi ya neema takatifu, sababu ulifukuza mitengo ya ufumu na ulinyenyekesha kiburi ya walozi katika mafundisho matakatifu ; na hivi uliongoza wote pa mito na pale ndani ya maji ulibatiza ma elfu mengi na hivi ulisabitisha Kanisa Orthodoksa ya Kongo.

 

Inafurahi leo Kanisa Takatifu kwa ukumbusho yako, ewe Mtume na musharufu Kosmas, kwani, sawa ilifai, aliweka kichwani chako takatifu taji ya utukufu na anasifu mashindano yako yenye uliyavumilia ili ya kuzambaha kati ya mateso, Imani yetu takatifu, iliyosabitisha pa damu yako, iiliyomwangwa njiani kwa Imani ya Kristu.

 

Nani ataweza kuhimidi, ewe mwenye akili wa Mungu, mashindaji yako mengi, ambaye uliyavumilia kwa upendo ya Kanisa ya Muumba ? Namna gani ulisimamisha Imani katika maneno yako matakatifu ; namna gani ulikombanisha wakosefu ya imani ; Basi na sisi, ewe padri, tunakusifu wote na tunakuomba utusaidie kwa maombi yako yenye uwezo.

Utukufu kwa Baba…Sauti ya tano.

Ni kweli ya kama imezambahwa pa ulimwengu nzima neno ya matendo yako, ewe mtume wa Kristu Kosmas. Mataifa, makabila na ma ulimi ya Afrika nzima wanatukuza katika furaha michoko yako yasipo semwa, ma safari yenye siku na usiku kwa tendo ya Mungu, jengo ya ma Altari mengi kwa utukufu ya Mungu, ma nyumba ya wenye yatima, ma obitalo ya wagonjwa, ma kimbilio ya wafungwa na ulinzi yako ya kila mtu mwenye mateso. Kwa hivi, ewe rafiki wa Kristu na ndugu wetu mupenzi na baba wa roho ilionekana kabisa, ile siku ya mauti yako, kwa nini walikuja ku maziko yako ma elfu mengi ya watu juu ya kukusalimia katika mashukuru yao mengi. Kwani na sisi tunakushukuru kwa upendo yako, tunakuomba utukumbuke pamoja na majeshi ya Wamalaika na Watakatifu wote pale mbinguni na ongoza mwendo yetu kwa kutimiza ma amri yako na kufuata mashindano yako, ewe mwenye heri kamili Padri wetu mkubwa.

Sasa na siku zote….Theotokion.

Sisi waaminifu tunakutaja mwenyi heri, ee Bikira Mzazi-Mungu, na tunakutukuza kama inavyofaa, muji imara, boma isiyoweza kuharibika, mlinzi muhodari na kimbilio ya roho zetu.

 

 

DOKSOLOGIA KUBWA NA KUAGA

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

PARAKLISIS

 

(KANUNI YA KUSIHI) YA MTAKATIFU SHAHIDI NA MTUME KOSMAS GRIGORIATIS

MTUME MKUBWA YA KONGO

       

Tafsiri: Mutawa Damaskinos Grigoriatis

 

 

Padri anabariki: Ahimidiwe Mungu…, msomaji:

 

Zaburi 142

Sikia maombi yangu, ee Bwana, usikilize kusihi kwangu;  katika uaminifu wako unijibu, katika haki yako. Usihukumu mutumishi wako;  maana machoni mwako hakuna mutu aliye hai atahesabiwa haki. Maana adui amefuata nafsi yangu;  amepiga uzima wangu chini hata udongo. Amenikalisha katika pahali pa giza, kama wale waliokufa zamani. Kwa hivi roho yangu imezimia ndani yangu;  Moyo wangu ndani yangu ni ukiwa. Ninakumbuka siku za kale;  ninafikili matendo yako yote;  ninawaza kazi ya mikono yako. Ninakunyoshea mikono yangu;  nafsi yangu inaona kiu kwa wewe, kama inchi inayochoka. Fanya mbio kwa kunijibu, ee Bwana;  roho yangu inazimia;  usinifichie uso wako;  nisiwe kama wao wanaoshuka shimoni. Unifanye kusikia wema wako asubui;  kwa maana ninakutumainia wewe;  unijulishe njia nitakayoikwenda;  kwa maana ninakunyanyulia nafsi yangu. Uniponyeshe, ee Bwana, na adui zangu, ninakukimbilia unifiche. Unifundishe kufanya mapenzi yako;  kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu;  Roho yako ni mwema;  uniongoze katika inchi ya haki. Unipatize uzima, ee Bwana, kwa ajili ya jina lako;  kwa haki yako utoe nafsi yangu katika taabu. Na kwa wema wako ukatilie mbali adui zangu, na kuwaharibu wote wanaotesa nafsi yangu;  kwa maana mimi ni mutumishi wako.

 

Kisha waimbaji wanaimba: Bwana ndiwe Mungu….Kisha:

Sauti ya inne. Mfano: O ipsothis en to Stavro.

Kujeni katika upendo na furaha ya roho kwa kumusihi sasa Kosmas mletaji Mungu, mtume mkubwa ya Afrika yenye Kati, aliyemaliza ushuhuda yake ya kumwanga na damu yake mjini Kolwezi ya Kongo. Kwa hivi tuseme nguvu kwake , salamu rafiki ya Watakatifu wote.

Utukufu…mara ingine

Sasa na siku zote…Theotokion

Sisi tusiyostahili hatutanyamaza, kusema kamwe uwezo wako ee Muzazi-Mungu. Kama wewe hungepatamisha kwanza, nani angetuokoa toka hatari mingi?  Nani angetuchunga huru, mupaka sasa?  Hatutaondoka mbali nawe, ee Bibi Malkia, kwani unaokoa  daima watumishi wako toka  mateso.

 

Tunasoma: Zaburi 50. 

Unirehemu, ee Mungu, sawasawa na wema wako;  sawasawa na wingi wa rehema  zako uzime makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, na kunisafisha  na zambi yangu. Maana ninajua makosa yangu, na zambi yangu ni mbele  yangu daima. Nimekukosea wewe peke yako, na kufanya yaliyo mabaya machoni  mwako;  ili ujulikane kuwa mwenye haki wakati unaposema, na kuwa safi  wakati unapotea hukumu. Tazama, niliumbwa katika hali ya uovu;  na  katika makosa mama yangu alinichukua mimba. Tazama, wewe unataka kweli  moyoni, na kwa siri utanijuulisha hekina. Unisafishe kwa hisopo na  nitakuwa safi;  unioshe, na nitakuwa mweupe kupita theluji. Unifanye  kusikia furaha na shangwe;  ili mifupa uliyovunja ifurahi. Ufiche uso  wako usitazame zambi zangu;  na uzima maovu yangu yote. Umba moyo safi  ndani yangu, ee Mungu, na ufanye eupya roho nzuri ndani yangu. Usinitenge  na uso wako, wala usiondolee Roho yako Mtakatifu. Unirudishie furaha  ya wokovu wako;  unitegemeze kwa roho ya tayari. Halafu nitafundisha  wenye makosa njia zako;  na wenye zambi watarudi kwako. Uniponyeshe  na damu ya watu, ee Mungu, wewe Mungu wa wokovu wangu;  ulimi wangu  utaimba na sauti haki yako. Ee Bwana, ufungue midomo yangu, na kinywa  changu kitaonyesha sifa zako. Maana hupendezwi na zabihu, ao ningeitoa, huvunjika, moyo uliovunjika na wa toba hutauzarau, ee Mungu. Utendee  Sayuni mema kwa mapenzi yako, ujenge kuta za Yerusalema. Halafu utafurahi  kwa zabihu za haki, kwa sadaka ya kuteketezwa, na sadaka nzima ya  kuteketezwa;  halafu watatoa ngombe ndume juu ya masabahu yako.

 

Kisha hii Zaburi, tunaanza kuimba  hii Kanuni:

 

WIMBO YA KWANZA     Sauti ya Mnane. Mfano : Igran diodefsas

 

WIMBO YA KWANZA

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Ulionekana kama nyota  muda hiyo wa sasa, ewe mwimbiwa Padri, Kanisani wa Kristu, kwa kutufundisha na kutuletea zawadi ya kitubio kwa mahubiri yako.

 

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Tunapiga magoti sisi wote kaburini yako takatifu na tunaomba daima matone ya upendo ya neema yako, tena na tunzo ya magonjwa yetu.

 

Utukufu kwa Baba…

Ulitukuza katika matendo yako, Utatu Mtakatifu ndani ya Shamba ya Kanisa ya Afrika na ulivuna matawi yasipokauka na unasali kwa wale wanakimbilia kwako daima.

Sasa na siku zote….Theotokion.

Angalia, ewe Mama Mwema, na sikia maombi letu, tena shusha nguvu ya ma tamaa yetu, juu hivi na sisi tunakuhimidi kama Bibi Malkia Mwimbiwa kamili.

 

Nyimbo ya tatu. Ouranias apsidos.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Kundi ya wapadri wako, waaminifu wingi ya wenye Afrika, wanakuja kaburini yako na katika furaha wanakusujudu na wanaomba katika upendo ya roho yao, ukombozi ya matendo mabaya toka kila taabu.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Kwa sababu tunachunga huku ya Afrika kweli mwili yako, pahali katika matendo yako yenye uhodari ulimutukuza Mungu, tunakaribia kwako, kwa kutupatia neema ya uponyo, ile Mungu alikupa nyingi kwako.

Utukufu kwa Baba…

Inashangilia inchi yako Ungiriki kwa uzalio yako pale, tena na mji Thesaloniki inafanya karamu na monasteri ya Grigoriu ya Mlima Athosi inakusifu na inatukuza mashindaji yako matakatifu, ewe mwenye heri.

 

Sasa na siku zote….Theotokion.

Hatuweze, ewe Mama Mwema, tusimamishe muto ya majaribu, bila saidio yako; basi tunavumilia kuja na haraka kutuokoa toka mitengo ya mwovu shetani kwa ajili ya saidio yako kubwa.

 

Okoa, wale wanatembea siku na usiku na  wanapata hatari kwa ajili ya vishawishi ya maisha. Na ponyesha wagonjwa wote.

 

Tazama kwa fazili, Muzazi-Mungu Musifiwa-kamili, katika taabu ya mwili wangu, na ponyesha maumivu ya nafsi yangu.

 

PADRI: Utuhurumie, ee Mungu, kadiri ya huruma yako kubwa, tunakuomba utusikia na ukatuhurumie.

Waimaji:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Tena tunakuomba kwa ajili ya Wakristu Waorthodoksi wote.

Waimaji:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Tena tunakuomba kwa ajili ya Askofu Mkubwa wetu (jina lake).

Waimaji:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Tena tunakuomba kwa ajili ya Mapadri wetu na kwa ndugu wetu wote katika Kristu.

Waimaji:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Tena tunakuomba kwa ajili ya kupata rehema, uzima, amani, afya, wokovu, ulinzi, usamehe na ondoleo ya zambi za watumishi wa Mungu, wadini wetu na Wakristu    Waorthodoksi ambao wanakaamo na na wanakutana katika muji huu (Monasteri ao Mission, Parokia) wawakili na wapotani wa Hekalu hii Takatifu na ya watumishi wa Mungu. . .

Sasa padri anasoma majina ya wahai.

WAIMBAJI:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Kwa kuwa wewe ndiwe Mungu wa huruma na mpenda-wanadamu na kwako tunautoa utukufu kwa Baba, na kwa Mwana, na kwa Roho Mtakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele. 

MSOMAJI:  Amina.

KATHISMA   Sauti ya mbili. Presvia thermi

Kama umande na hewa ya baridi, unaonekana kati ya wenye kuteswa na unawatoa tengenezo ya makosa yao; tena unawasabitisha, ewe mwenye heri, katika bunduki ya imani na unawapandisha pa mwendo yenye kiroho. Kwa hivi, sisi wote tunatukuza katika masifu michoko na majashu yako.

 

Nyimbo ya ine. Isakikoa Kirie.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Sasa sikia waaminifu wako, wenye wanakuja katika heshima daima kw akusujudu kama hazina takatifu na yenye kujaa na ma zawadi kaburi yako heshimiwa.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Fukuza giza ya mateso yangu na upiganaji ya ma zoezo yanhu mabaya, kwani ninakimbilia kwa kifuniko yako, ewe Kosma, musaidizi ya sisi wote.

Utukufu kwa Baba…

Kwa kuhubiri neno ya wokovu, ewe Kosma, ulitembea na gari yako pa fasi ya mbalimbali juu ya kuongoza watu wenye Afrika njiani ya ukombozi.

Sasa na siku zote…Theotokion.

Kila siku na usiku, tunakimbilia kwako, ewe Mwimbiwa kamili, juu ya kupata ukombozi toka magumu na mitengo ya mwovu shetani.

 

Nyimbo ya Tano. Fotison imas.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Zimisha nguvu ya ma shetani na ukamio ya wa adui wetu, katika maombi yenye nguvu yako na utuongoze, ewe mwenye hekima, bandarini ya wokovu.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Utukumbuke ma siku hizi ya kukosa kitumaini yetu, na utumwange neema ya furaha, sawa unakaa na uwezo mbele ya Mungu, ambaye ulimutukuza na matendo yako.

Utukufu kwa Baba…

Ewe mwenye hekima, fukuza bahari ya ma tamaa yangu kwa bahari ya maombi yako mtakatifu, na haribisha mitengo ya ufumu na utuokoe sisi wote.

 

Sasa na siku zote….Theotokion.

Angaza ma roho yangu na haribisha koti ya mawazo yangu mabaya, sawa ni Mwimbiwa kamili, mnara ya ulinzi kwa wale wanakimbilia na kitumaini kwako.

 

Nyimbo ya  sita. Ilasthiti mi Sotir.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Ulitembea kweli ma njia mengi ya inchi Kongo, ewe mwenye heri, na ulimukombanisha shetani siku na usiku na yoyote mitengo yake kwa ukombozi ya watoto war oho yako.

Mtakatifu wa Mungu Kosma, utuombee.

Tunasifu katika heshima kulala kwako takatifu, ile ulipata njiani kwa mushimbi, ewe Mutawa Kosma, na hivi ulimutukuza Mungu; tena ulitukuzwa kwa Huyu kwa kutenda miujiza yenye ajabu.

Utukufu kwa Baba…

Tosha mbali mateso ya waaminifu wako wenye Afrika na uwape furaha; tena tengeneza matatizo yao na uje na haraka pa gazabu yao, ili wote watakutukuza daima.

Sasa na siku zote…Theotokion.

Aliingia kwako, ewe Bibi-Malkia mujaliwa neema kwa Mungu, Neno wa Mungu, aliyefanyika Mutu kwa kuhamusha toka uharibifu kizazi ya watu kwa kupata uzima ya milele.

 

Okoa, wale wanatembea siku na usiku na  wanapata hatari kwa ajili ya vishawishi ya maisha. Na ponyesha wagonjwa wote.

 

Tazama kwa fazili, Muzazi-Mungu Musifiwa-kamili, katika taabu ya mwili wangu, na ponyesha maumivu ya nafsi yangu.

 

KONTAKION

Sauti ya mbili. Ta ano ziton.

Kwa sababu ulimupenda Kristo tangu umri utoto yako, ewe Mwenye heri kamili,  ulimufuata katika upendo na ulisikia sauti yake kwa kutembea pa lupango ingine Yake juu ya kumuhubiri  kwa wokovu ya wale wanaishi ndani ya giza.

 

PROKIMENON

Sauti ya ine.

Mafundisho yao yalisikilika duniani kote na neno lake mpaka mwisho wa dunia. (mara tatu)

Shahiri: Mbingu zinahadisia utukufu wa Mungu, anga inatangaza kazi ya mikono yake.

 

PADRI:  Tumusihi Bwana Mungu wetu atustahilishe kusikiliza Evangelio Takatifu

MSOMAJI:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Hekima.  Inukeni, tusikilize Evangelio Takatifu.  Amani kwa wote.

MSOMAJI:  Na kwa roho yako.

PADRI:  Somo la Evangelio Takatifu limeloandikwa na Luka.Tusikilize.

MSOMAJI:  Utukufu kwako, ee Bwana, utukufu kwako.

 

EVANGELIO TAKATIFU (Luka 9,1-6)

Yesu aliwaita wale Kumi na wawili wakusanyike, akawapa uwezo na amri juu ya mashetani wote na (nguvu ya) kuponya magonjwa. Akawatuma watangaze Ufalme wa Mungu na kuwaponya wagonjwa. Akawaambia: „Msichukue kitu kwa safari, wala bakora, wala mfuko, wala mkate, wala feza; wala msiwe kila mmoja na kanzu mbili. Tena mnapoingia nyumba yoyote, kaeni humo, na toka humo mtaondoka. Na kama watu hawawakaribishi ninyi, tokeni katika mji wao, kunguteni mavumbi ya miguuni mwenu, iwe ushahidi juu yao“. Basi wakaenda, wakazunguka kijiji kwa kijiji, wakihubiri Habari Njema na kuwaponyesha wagonjwa popote.

 

Waimbaji: Utukufu kwako, ee Mungu, utukufu kwako.

 

Utukufu kwa Baba….Kwa maombezi ya Mtume yako, ee Murahimu, uufute wingi ya makosa yetu.

 

Sasa na siku zote…Kwa maombezi ya Mzazi Mungu, ee Murahimu, uufute wingi ya makosa yetu.

 

Shahiri: Unirehemu, ee Mungu, sawasawa na wema wako kubwa;  sawasawa na wingi wa rehema  zako uzime makosa yangu.

 

Sauti ya sita. Olin apothemeni.

Zimisha mawimbi ya mfano mbaya ya ma shetani, haribisha mitengo ya waovu wa  adui  wakosefu ya imani yetu, utufunike katika maombi yako na ulinzi yako isiyolala, tena waka rohoni mwetu bidii takatifu ya upendo kimungu na utupandishe pa mwendo kwa kupanda mu uzima ya kiroho, ewe mletaji Mungu Kosmas, tena utusaidie kumupenda Kristu na hivi katika ma bunduki ya neema takatifu tupate na sisi zawadi ya wokovu yetu.

 

PADRI. Ee Mungu uwaokoe watu wako ukaubarikie urizi wako. Agua  dunia yako kwa huruma na rehema;  paza pempe ya wakristu waorthodoksi, ukakunjua juu yetu mafazili yako tele;  kwa ajili ya maombezi ya Maria  Bibi yetu msiye na doa. Mzazi-Mungu na Bikira daima. Kwa nguvu ya Msalaba mheshimiwa na tukufu. Kwa matunzo ya majeshi yaheshimiwa ya  mbinguni yaliyo bila mwili. Kwa maombi ya Yoane Mtangulizi, Mbatizaji, Nabii, Mtukufu na Muheshimiwa. Ya Mitume Watakatifu, Watukufu na Wasifiwa.  Ya Wapadri wetu ambao katika Watakatifu na  Waaskofu na Walimu Wakubwa, Bazile Mkubwa, Grigori Mutheologo, Yoane Krisostomo, Athanasie na  Kirilli, Yoane Mrahimu, wapatriarka wa Aleksandria, Nikolao wa muji Mira, Spiridon Askofu Trimithunta wa miujiza, ya Mashahidi Watakatifu  watukufu na washindaji wazuri;  ya wapadri Watawa na Wabebaji-Mungu;   ya Mashahidi Watakatifu watukufu wakubwa, ya Georgio  Mumebaji ya ushindi, Dimitri mwenye kutosha manukato, Theodoro Mukubwa wa askari na Theodoro  Jemadari;  ya Mababu-Mungu  Watakatifu na wenye haki Yoakimu na Anna;  ya Mtakatifu (anataja jina  na majina ya kujulisha mtakatifu wa siku ile) aliye tunamukumbuka leo  hata na Watakatifu wako wote pamoja, Tunakusihi, ee Bwana, uliye  peke yako na huruma kubwa, usikie sisi watu wenye zambi tukikuomba  na ukatuhurumie.

 

MSOMAJI:  Bwana, hurumia (mara 12). 

PADRI:  Kwa kurehemu, na huruma, na upendo-wanadamu wa Mwana  wako wa pekee, pamoja naye Uhimidiwa, pamoja na Roho wako Mtakatifu  kamili, Mwema, Mpaji-uhai, sasa na siku zote, hata milele na milele.

MSOMAJI:  Amina.

 

Nyimbo ya saba. I ek tis Ioudeas

Mtakatifu Mtume wa Mungu, utuombee.

Makundi ya waaminifu wanakuhimidi, ewe Padri, na wanaomba msaada yako takatifu, uwezo ya matunzo na ongezeko ya kitumaini; hivi watakusifu daima, sawa mulinzi na mkombozi.

Mtakatifu Mtume wa Mungu, utuombee.

Katika upendo ya Muumba ulionyeshwa mulinzi ya waaminifu ya Afrika na mwalimu wa wote; basi katika upatanisho yako tunza ku magonjwa wale wanayoteswa toka ma gazabu na magumu na kwa taabu ya makosa yao.

Utukufu kwa Baba…

Ewe mwenye hekima, kwa ajili ya ushuhuda na kumwangisha damu yako ulitukuzwa; basi sasa unamutukuza Rabi na sisi katika wimbo tunakusifu sawa mushindaji mtakatifu na rafiki ya Watakatifu.

Sasa na siku zote….Theotokion.

Tangu umri ujana yangu, ewe Mama, nilifanyikwa bahati mbaya, mtumwa ya ma shetani na joaka kwa ajili ya mitengo mabaya; basi ewe Bibi-Malkia, uniokoe na haraka toka zoezo ya zambi na hivi nitakuhimidi na heshima.

 

Nyimbo ya mnane. Ton Vasilea.

Mtakatifu Mtume wa Mungu, utuombee.

Usizarau mataifa ya wenye Afrika, wenye wanakimbilia kwako na katika nguvu yao wanaomba tunzo ya magumu ya maisha yao.

Mtakatifu Mtume wa Mungu, utuombee.

Ewe Padri, fukuza chuki mbaya ya watumishi ya shetani na utupe ukombozi na wokovu kwa kila ugomvi yao.

Utukufu kwa Baba…

Ulionekana kweli wewe pa mstari umoja ya Mitume, sababu ulihubiri miujiza na Kristu pa hizi miaka yenye mwisho shambani ya Mungu huku ya Afrika.

Sasa na siku zote….Theotokion.

Uje na okoa, ewe Mama Bikira, kutoka vishawishi yote ya maisha wale wanakuja katika imani kwako na wanakutukuza kwa milele yote.

 

Nyimbo ya Tisa. Kirios Theotokon.

Mtakatifu Mtume wa Mungu, utuombee.

Kujeni katika upendo na mupige magoti mbele ya kaburi yake na museme, ewe padri Kosma, linda na funika sisi toka magumu yoyote.

Mtakatifu Mtume wa Mungu, utuombee.

Kwani unakaa na uwezo ma siku hizi yenye mwisho, sikia maombi yetu sasa na utupatie matunzo tele, ewe mtakatifu wa Mungu.

Utukufu kwa Baba…

Waaminifu wenye Ungiriki, pamoja na makundi ya wakristu ya wenye Afrika, ewe Kosma Padri, wanakuhimidi na, katika upendo wanakimbilia wote kaburini yako.

Sasa na siku zote…Theotokion.

Katika upatanisho yako, ewe Binti wa Mungu, fukuza mitengo ya ma shetani na ya wa adui yetu, na tena utupe tele mwangaza ya neema yako takatifu.

 

Ni wajibu kweli….

Kujeni tukimbilie sisi waaminifu kaburini ya shahidi Kosmas ili kusujudu katika heshima na kutoka roho yetu na kutosha machozi tuombe bahari ya matunzo na tumushukuru na shangwe.

 

Ma kundi ya waaminifu wote toka mji Thesaloniki na ya ma muji ya Kongo Afrika mufurahi sasa na shangwe, kwani muna kweli Kosmas mletaji wa Mungu, mulinzi na mutungaji na mushindaji ya imani takatifu.

 

Muji Kolwezi ya Afrika Kongo, na jibo yote ya Katanga sasa inatukuza mashindano yako matakatifu,   yaliyovumilia, ewe mletaji Mungu, kwa usabitisho ya Kanisa wa Kristu.

 

Ma kundi ya wagonjwa kwani walipata ma gazabu ya maisha yao, wanakimbilia ma siku zote kaburini yako na katika upendo wanaomba tunzo ya kila ugonjwa yao na ukombozi ya ma nafsi zao.

 

Monasteri ya mtakatifu Grigorio ya Mlima Athosi kuwa na furaha, kwani inachunga musaidizi mwenye angaza, mwalimu Kosmas, mutungaji ya Afrika nzima na mkombozi mbele  ya kila uhitaji na jaribu kubwa.

 

Kujeni waimbaji ya Waorthodoksi na warafiki ya Watakatifu, tumuhimbie katika heshima huyu aliyepanda pa mstari moja ya Mitume wa Kristu na mwenye muujiza, Kosma mutukuzwa.

 

KITUKUZO YA MWISHO

Majeshi yote ya Malaika, Mtangulizi wa Bwana, Mitume Kumi na mbili, Watakatifu wote pamoja na Mzazi-Mungu, mupatanishe kwa ajili, ya wokovu wetu.

 

Elezo: Matukuzo ya siku ya Juma.

 

 

 

 

 

 

 

MATUKUZO YA MA SIKU YA JUMA

 

SIKU YA KWANZA

Kujeni enyi waaminifu wote, tuwasifu nyota mbili, wakubwa nawaangaza, Mikaeli Mkubwa na Gavrieli Kimungu, Wajemadari wawili wa Mungu mwenyezi.

SIKU YA PILI

Mutangulizi wa Bwana na Mubatizaji, bakuli mbele ya jua, nyota ya asubui, kwa mwangaza wako, angaza nafsi yangu, nyonge na kipofu kwa tamaa mbaya.

SIKU YA TATU NA YA TANO

Naimba usulubisho wako, ee Mwema, naimba mateso yako, na kusujudu maziko yako, tete, misumari, mukuki, sifongo, naisujudu yote, Mwokozi Muvumilivu.

KATIKA SIKU YA INE

Tunasifu kwa nyimbo Petro, Pavlo, Marko, Luka, Filippo, Matayo, Yoanne, Simona na Tomasi, Andrea Mutukuzwa, pamoja na Yakovo, na Bartolomeo.

 

Sisi wote tumusifu Muierarkha, wa maajabu, na Musaidizi asiyeshindwa, katika lazima, Muchungazi Mtakatifu, padri wa Bwana, Nikolao Mkubwa.

 

SIKU YA POSHO

Kwa maombi ya Mitume yako, ya Manabii, ya Mashahidi, ya Waierarkha na ya Watawa, ewe Murehemu na Mwema-Kamili, leta upumuziko kwa nafsi uliopokea.

 

MSOMAJI:  Mungu Mutakatifu. Mweza Mutakatifu. Musiye kufa Mutakatifu. utuhurumia. (mara tatu).  Utukufu kwa Baba.  . .   Sasa na siku zote.  . .   Utatu Mutakatifu.  . .   Utukufu kwa Baba.  .  Sasa na siku zote.  .  Bwana hurumia  (mara tatu).  

Baba yetu uliye mbinguni.  . .   

PADRI:  Kwa kuwa. . .

WIMBO   Sauti ya mbili

WAIMBAJI:  Utuhurumie, ee Bwana, utuhurumie, kwa kuwa sisi watu wenye zambi, hatuna teto yoyote kukuileta, ila ombi huu tunakutolea kwako, uliye Rabi, utuhurumie.

Utukufu kwa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu.

Ee Bwana, utuhurumie, kwa kuwa tunategemea kwako. Usituazibu sana, wala kuzikumbuka zambi zetu. Lakini hata sasa utangalie, kama mwenye huruma, ukatuokoe na maadui wetu. Kwa kuwa wewe u Mungu wetu, tena sisi watu wako. Sisi zote viumbe vya mikono yako;  jina lako tunaliita.

Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.

Utufungulie mulango wa huruma, ewe Muzazi-Mungu mubarikiwa. Tukikutumaini wewe, tutakuwa bila kuanguka. Kwako tutaziepuka taabu;  Kwa kuwa wewe  wokovu wa muzao wa wakristu.

 

PADRI: Utuhurumie, ee Mungu, kadiri ya huruma yako kubwa, tunakuomba utusikia na ukatuhurumie.

Waimaji:  Bwana hurumia (mara tatu).

PADRI:  Tena tunakuomba kwa ajili kuchunga muji huu (ao Monasteri ao Mission) na muji na migini yote, toka gazabu, njaa, majonjwa ya kuambukiza, tetemeko la inchi, garika, moto, upanga, ushambulio ya watu wageni, magombano, kufa musiba, kwa ajili ya Mungu wetu na mpenda-wanadamu awe Murehemu.  Mwema na Mupendwa, kusudi afukuze na asambaze kila gazabu na magonjwa inayokaribia juu yetu, na akomboe sisi toka makanio yake mwenye haki na atuhurumie.

 

Msomaji:  Bwana hurumia (mara makumi ine).

PADRI:  Utusikilize, ee Mungu Mwokozi wetu, kitumaini ya mwisho wa inchi, na bahari mbali.  Na awe murehemu sana kwetu, ee Rabi, kwa ajili ya zambi zote, hata milele na milele.

MSOMAJI:  Bwana hurumia (mara tatu).

 

PADRI:  Kwa kuwa ewe Mungu murehemu na mpenda-wanadamu, na kwako tunautoa utukufu kwa Baba na kwa Mwana, na kwa Roho Mutakatifu, sasa na siku zote, hata milele na milele.  Amina.

MSOMAJI:  Utukufu kwa Baba.  .  Sasa na siku zote.  .  Bwana hurumia  (mara tatu).  Ee Rabi Mtakatifu, bariki.

PADRI:  Kristu Mungu wetu wa kweli, kwa maombezi ya mama yake Mtakatifu asiye na doa wala si la wama kamili, kwa uwezo wa Musalaba Muheshimiwa na muhishaji, kwa kusihi ya Mashahidi watakatifu, Watukufu, Washindaji wazuri, ya Wapadri wetu waaskofu na Walimu Wakubwa, ya Wapadri wetu Matawa na Wabebaji-Mungu, ya Yoakimu na Anna, Mababu-Mungu Watakatifu na wenye haki, ya (anataja jina la Mutakatifu wa siku ile), aliye tunamukumbuka leo, hata na Watakatifu wote, atuhurumie, akatuokoe yu Mungu Mwema, Murahimu na mpenda-wanadamu.

 

Tena tunaimba wimbo wa Mwisho na watu wanasujudu Picha ya mtakatifu

 

WIMBO WA MWISHO

Sauti ya Pili. Ote ek tou ksilou

Makundi yote ya warafiki ya ma siku Kuu na wenye wingi ya wagonjwa, kujeni tufike na kusujudu picha takatifu yake na tupige magoti kaburini yake  na kumuombea atutunze kwa kila ugumu. Basi, ewe Kosma, mwenye kuangazwa kwa Mungu, utulinde kwa kila hasira ya ma shetani, ya kila gazabu na chukizo na utupe uponyo ya magonjwa na kila saidio kwa wale wanakimbilia daima kwako katika imani.

 

INGINE. SAUTI UMOJA.

Ulishuhudiwa musaidizi ya watu wote na muganga ya wagonjwa, tena mutawa mushndani na mwenye hekima, sawa uliishi shambani ya Afrika nzima, pahali ulmukombvanisha mwovu shetani na uliharibisha kiloa kitengo ya ulozi kwa ajili ya uzima yako takatifu. Basi, kweli ulionyesha nhguzo ya Orthodoksia, ewe mwenye akili wa Mungu na musaidizi ya wa ndugu wako wenye Afrika.

 

Sauti ya mnane.

Bibi Malkia pokea kusihi, na watumishi wako, na utukomboe, toka kila lazima na sikitiko.

Sauti ya mbili.

Ninakuelezea kitumaini yangu yote, ee Mama wa Mungu, unilinde chini ya kivuli chako.

 

Kwa maombezi ya wapadri wetu watakatifu, ee Bwana Yesu Kristu Mungu wetu, utuhurumie.  Amina.

 

14-8-2018

Mutawa Damaskinos Grigoriatis

  

Μέ τήν εὐλογία τοῦ πατρός Δαμασκηνοῦ Γρηγοριάτου